Wednesday, July 9, 2014

Uholanzi yatupwa nje....


Timu ya Argentina imefuzu kwenda fainali baada ya kuifunga timu ya Uholazi na  kuondoa matumaini yao ya kuweza kunyakuwa ubingwa huo. Timu hizo zilitoka suluhu katika dakika zote na ndipo muda wa penati ulipowadia na timu ya Argentina kupata penati 4 dhidi ya 2 walizopata Uholanzi.

Fainali itakuwa ni kati ya Ujerumani dhidi ya Argentina baada ya hapo jana Ujerumani kuipiga Brazil kipigo cha mbwa mwitu kwa magoli 7 - 1 nakuondoa matumani ya Brazil kulibakisha kombe hilo nyumbani.


0 comments:

Post a Comment