Tuesday, July 1, 2014

Halmashauri zote zaagizwa kuendelea na matayarisho ya uchaguzi


 Waziri mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda ameziagiza halmashauri za wilaya nchini kuendelea na matayarisho ya uchagauzi mkuu wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu huku jitihada zikifanywa na serikali kuwaomba umoja wa katiba ya wananchi  -Ukawa kukubali kuridhia ombi la kurudi bungeni ili azma hiyo iweze kufikiwa.

Mheshimiwa Pinda ametoa agizo hilo wakati akizungumza na wakurugenzi, wenyeviti na viongozi wa serikali ngazi ya taifa katika kikao cha pamoja kilichofanyika jijini Tanga.
Amesema kama kutakuwa na mabadiliko kuhusu kuahirishwa kwa uchaguzi huo huku pande zote mbili zikirudi kuendelea na bunge la katiba viongozi hao watapewa taarifa kuhusu mchakato huo lakini matayarisho ya uchaguzi mkuu wa serikali za mitaa ni lazima yafanyike.
Kuhusu uwekezaji waziri mkuu ameziagiza halmashauri za wilaya nchini kuhakikisha kuwa wanatangaza fursa za uwekezaji zilizopo katika maeneo yao kama walivyofanya mkoa wa Tanga mwishoni mwa mwaka jana ambapo walifanya kongamano la uwekezaji lililoshirikisha wawekezaji wa ndani na nje ya nchi hatua ambayo imeanza kuleta mafanikio kwa Tanga na taifa kwa ujumla.

0 comments:

Post a Comment