Tuesday, July 1, 2014

Serikali inaendelea na maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za mitaa


Waziri Mkuu MIZENGO PINDA amesema serikali inaendelea na maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika nchini mwezi Oktoba mwaka huu.

Akizungumza mkoani TANGA na mameya wa majiji, manispaa na wenyeviti wa Halmashauri za Miji na Wilaya nchini, Waziri Mkuu PINDA amesema hata hivyo hatma ya kufanyika kwa uchaguzi huo inategemea kukamilika kwa mchakato wa Katiba mpya.

Waziri Mkuu amesisitiza suala la ukusanyaji mapato na udhibiti wa matumizi ya fedha za serikali na kuongeza kuwa amewaandikia barua Wakuu wa Mikoa akiwataka waweke utaratibu wa kutoa taarifa kila baada ya miezi mitatu juu ya makusanyo ya kila Halmashauri zilizo kwenye mikoa yao.

0 comments:

Post a Comment