Wednesday, July 2, 2014

Serikari kutaifisha mashamba yasiyoendelezwa Tanga.


Waziri mkuu mheshimiwa Mizengo Pinda ameuagiza uongozi wa serikali mkoa wa Tanga kuorodhesha mashamba yote yasiyoendelezwa kisha kuwasilisha kwake ili aweze kumkabidhi mheshimiwa Rais aweze kutoa maamuzi kufuatia baadhi ya wawekezaji kuhodhi maeneo makubwa na kusababisha wananchi kukosa mashamba ya kulima.
Mheshimiwa Pinda ametoa agizo hilo wakati akihutubia mamia ya wakazi wa mkoa wa Tanga katika kilele cha maonesho ya biashara ya halmashauri zote nchini yaliyofanyika kitaifa jijini Tanga kisha washindi kukabidhiwa tuzo kama ishara ya kuvutia wawekezaji.
 
Kuhusu mchakato wa uchaguzi mkuu ujao waziri Pinda amewaagiza viongozi wa kuanzia serikali za mitaa na vijiji,kata,tarafa hadi wilaya na taifa kwa ujumla kuwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa kuchagua viongozi wenye sifa katika uchaguzi mkuu ujao wa serikali za mitaa ili kulinda Demokrasia ya kweli kwa watanzania.
 
Awali mwenyekiti wa jumuiya ya tawala za serikali za mitaa nchini (ALAT) Dr,Didas Masaburi amesema jumuiya haitamuunga mkono mgombea kuanzia ngazi ya Rais,Ubunge na Diwani endapo atashindwa kusimamia mchakato wa ugatuaji madaraka kwenda kwa wananchi ili kuleta demokrasia ya kweli.
 
Katika hitimisho la maonesho ya biashara ya halmashaurio zote nchini waziri mkuu alitoa zawadi kwa washiriki washindi wa maonesho hayo ambayo halmashauri ya jiji la Tanga iliibuka kidedea kwa kushika nafasi ya kwanza ikifuatiwa na halmashauri ya Bukoba.

0 comments:

Post a Comment