Wednesday, July 2, 2014

Wakazi wa Manyoni waiomba serikali kuwatatulia tatizo la maji.


Wakazi wa vijiji vya MAKALE, MITUNDU, MGANDU na ITIGI wilayani MANYONI mkoa wa SINGIDA wameiomba serikali kufanya juhudi za ziada kuwatatulia tatizo la maji katika maeneo yao.

Wakazi hao wamesema tatizo la maji limedumu kwa zaidi ya miaka 30 hali ambayo huwalazimu kukesha usiku kucha wakitafuta maji.

Wakazi hao wametoa kilio hicho mbele ya Naibu Waziri wa Maji AMOS MAKALA aliyetembelea vijiji mbali mbali wilayani Manyoni ili kukagua hali ya upatikanaji wa huduma ya maji.

Akijibu malamiko ya wananchi hao MAKALA amesema serikali inashughulikia tatizo la maji na hadi mwaka huu utakapokamilika tatizo hilo litakuwa limepatiwa ufumbuzi.


0 comments:

Post a Comment