Wednesday, July 2, 2014

NGORONGORO: Migogoro ya wafugaji kutatuliwa.



Waziri wa Maliasili na Utalii, LAZARO NYALANDU ameagiza bodi ya Mamlaka ya NGORONGORO kutatua migogoro ya wafugaji wanaoishi katika bonde la hifadhi ya NGORONGORO kufuatia wafugaji hao kufunga bara bara kwa madai ya kupinga kujengwa kwa hoteli ya kitalii katika hifadhi hiyo bila kushirikishwa.

Akizungumza na wafugaji hao Waziri NYALANDU amesema serikali haitaruhusu ujenzi wowote ufanyike katika eneo hilo kwa sasa mpaka hapo tathmini itakapofanywa na ofisi ya makamu wa Rais mazingira na kubaini iwapo ujenzi huo ufanyike au la.

Waziri Nyalandu ambaye alikwenda NGORONGORO kuzindua bodi mpya ya hifadhi ya NGORONGORO amesema ni vema bodi hiyo ikatafuta mbinu za kutatua migogoro katika sehemu ya hifadhi.

Kuhusu suala la uwakilishi zaidi wa wafugaji katika bodi ya NGORONGORO amesema ndani ya siku SABA atateuwa mwakilishi mwingine toka katika jamii hiyo ili aweze kuingia katika bodi hiyo na hivyo kufanya idadi ya wawakilishi WAWILI.

0 comments:

Post a Comment