Tuesday, July 1, 2014

Mwenge wa uhuru umeendelea na mbio zake katika mkoa wa NJOMBE


Mwenge wa uhuru umeendelea na mbio zake katika mkoa wa NJOMBE kwa kukimbizwa katika wilaya ya WANGING’OMBE ambako kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka huu RACHEL KASSANDA amewataka watanzania kuwapuuza wanasiasa wanaowapotosha wananchi wasishiriki katika shughuli za Maendeleo.

KASSANDA ametoa wito huo baada ya kuzindua, kufungua na kuweka mawe ya Msingi katika Miradi TISA ya maendeleo ambayo wananchi wa WANGING’OMBE wamechangia nguvu zao katika ujenzi wake.

Amesema watanzania wasikubali kuibomoa nchi yao bali wailinde waipiganie na kuitetea dhidi ya wanaoichafua

0 comments:

Post a Comment